Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Omari Mohamed Kigua

Primary Questions
MHE. OMAR M. KIGUA aliuliza:-
Ulipaji kodi ni chanzo kikuu cha mapato ya nchi kwa ajili ya maendeleo na Serikali inao wajibu mkubwa wa kuhakikisha kwamba wafanyabiashara, wakulima na wafanyakazi wanalipa kodi kwa mujibu wa sheria na ili Serikali iweze kukusanya kodi kwa ufanisi mkubwa ni lazima kuwe na Ofisi za TRA katika maeneo mbalimbali nchini:-
(a)Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Kilindi?
(b)Kwa kutokuwa na Ofisi za TRA Serikali haioni kama inadhoofisha maendeleo ya Wilaya hususani katika suala la mapato?
(c)Kwa kuweka Ofisi za TRA Wilaya ya Handeni na kuacha Wilaya ya Kilindi, Serikali haioni kama inawajengea wananchi tabia ya kukwepa kulipa kodi kutokana na umbali uliopo kati ya Wilaya hizo mbili?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Ili kuleta ufanisi wa kimaendeleo na kusogeza karibu huduma za kijamii kwa wananchi, Serikali hugawa Wilaya na Majimbo kwa kuangalia ukubwa wa eneo, idadi ya watu kwenye eneo husika, pamoja na shughuli za kiuchumi na Wilaya ya Kilindi ni miongoni mwa Wilaya chache zinazozalisha mazao ya kilimo na biashara kwa eneo kubwa:-
Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuligawa Jimbo hilo lenye ukubwa wa mita za mraba 6,125?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Moja ya Changamoto alizokutana nazo Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni katika Wilaya ya Kilindi ni tatizo la maji hususan maeneo ya Makao Makuu ya Wilaya, Kata za Saunyi, Mabaranga na kadhalika na Serikali ina Mradi wa Maji wa HTM ambao unatarajia kuwapatia jirani zetu wa Wilaya ya Handeni huduma ya maji ambapo utekelezaji huo utafanyika mwaka huu:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kufanya extension katika Wilaya ya Kilindi ili nayo ifaidike na mradi huu?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini kwa kutambua umuhimu wa wachimbaji wadogo wadogo imekuwa ikitoa ruzuku ili kuwawezesha wachimbaji kunufaika na madini yapatikanayo maeneo mbalimbali nchini:-
(a) Je, mpango huo umenufaisha wachimbaji wangapi nchini?
(b) Je, ni Mikoa na Wilaya zipi zinazonufaika na mpango huo?
(c) Je, Serikali ipo tayari kuweka utaratibu wa kuwakopesha wachimbaji wadogo wadogo ili kuwawezesha kuchimba madini?
MHE. OMARI M. KIGUA Aliuliza:-
Serikali imekuwa ikisisitiza na kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kulinda na kutunza vyanzo vya maji kwa kutokata miti ovyo na kutojenga karibu na vyanzo hivyo, lakini wako baadhi ya wananchi wenye tabia ya kushirikiana na baadhi ya watumishi wachache wa Serikali kukata miti ovyo na kujenga karibu na vyanzo vya maji.
(a) Je, ni lini Serikali itasimamia kikamilifu sheria za kulinda mito na miti nchini?
(b) Je, Serikali haioni umefika wakati sasa kutunga sheria kali zaidi ili kujihami na global warming?
MHE. OMARI M. KIGUA alijibu:-
Moja ya changamoto kubwa inayokabili maeneo mbalimbali nchini ni huduma ya maji safi na salama. Serikali kwa kushirikiana na mashirika ya kitaifa kama Benki ya Dunia wamekuwa wakitoa ahadi za kuwezesha miradi mikubwa ya maji nchini lakini mara nyingi wamekuwa hawatekelezi ahadi zao.
Je, Serikali haioni sasa imefika wakati wa kuweka mikakati ya dhati ya kutenga bajeti kwa kutumia mapato ya ndani ili kutoathiri miradi ya maji?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Mwaka 2014 Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Makao Makuu ya Wilaya ya Kilindi hadi Wilaya ya Gairo.
Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi hiyo?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Je, Serikali ipo tayari kutuma timu ya tathmini ya kukagua Miradi ya Maji ya Kwediboma, Kwekivu, Sange, Chamtui na Mafuleta ili kuona kama vigezo na viwango vya ujenzi wa miradi hii mikubwa vimezingatia thamani ya fedha (value for money audit)?
MHE. OMARI A. KIGODA - (K.n.y. MHE. OMARI M. KIGUA) aliuliza:-
Wilaya ya Kilindi ni miongoni mwa Wilaya chache zinazopata mvua nyingi nyakati za mvua lakini maji hayo yamekuwa yakipotea:-
• Je, Serikali ipo tayari kuweka utaratibu wa kuvuna maji hayo kwa kujenga mabwawa makubwa ya kuhifadhia maji hayo kwa matumizi ya binadamu?
• Je, Serikali imejipangaje kujenga mabwawa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na ufugaji wa samaki?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Serikali ya Awamu ya Tano inatoa elimu bure hali iliyosababisha wananchi wengi kupeleka watoto wao shule, huku ufaulu wa wanafunzi kuingia kidato cha tano ukiongezeka:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kila wilaya kuwa na Shule za Kidato cha Tano na Sita kuwa ni wa lazima hasa ikizingatiwa kuwa kuna baadhi ya wilaya hazina shule hizo?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-

Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za sekondari na za msingi nchini:-

Je, ni lini Serikali itafanyia ukarabati Shule za Sekondari Masagulu, Lwande, Mkuyu na Shule za Msingi Songe na Masagulu zilizopo Wilayani Kilindi?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-

Kwa muda mrefu sasa Wilaya ya Kilindi haina Hospitali ya Wilaya lakini wanayo Hospitali ya Rufaa inayomilikiwa na Kanisa la KKKT, lakini watumishi wote na huduma zote za Hospitali hiyo zinagharamiwa na Halmashauri ya Wilaya (DED) na wao KKKT ni wamiliki wa majengo:-

Je, Serikali haioni imefika wakati wa kufanya makubaliano ya kununua Hospitali hiyo ili kupunguza gharama kwa Serikali ya kujenga Hospitali ya Wilaya?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-

Serikali imekuwa na utaratibu wa kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa Mahakama za Mwanzo:-

Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Mahakama za Kata za Kimbe, Kwekivu na Kata ya Mswaki ambazo zimechakaa sana?
MHE. OMARI M. KIGUA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza ahadi ya muda mrefu ya ujenzi wa barabara kutoka Kilindi kwenda Gairo kwa kiwango cha lami?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaanza mkakati wa kusambaza maji kutoka Mto Dibuluma kata ya Kibati Wilaya ya Mvomero na kuyasambaza katika kata ya Tunguli, Kwekivu, Masagalu na Songe Wilayani Kilindi?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Wilaya ya Kilindi na Kiteto kupitia Kijiji cha Sambu?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Gari la Wagonjwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Handeni – Kiberashi – Kiteto – Chemba hadi Singida utaanza?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaondoa wananchi waliovamia Msitu wa Bondo uliopo Kata ya Mswaki, Kijiji cha Mswaki?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Kilindi?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya wagojwa katika Wilaya ya Kilindi?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Kilindi?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Kata ya Bokwa na Songe Kilindi?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapandisha hadhi barabara ya Kwinji - Kilindi Asilia hadi Kimbe?
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's