Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Mattar Ali Salum

Primary Questions
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-

Kikosi cha Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) huandaa vijana kwa mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kusubiri ajira katika vikosi vya ulinzi vya Muungano:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani madhubuti wa kutoa ajira kwa upande wa Tanzania Zanzibar?
(b) Je, ni asilimia ngapi ya vijana wanaoajiriwa kutoka upande wa Zanzibar?

(c) Je, kwa nini utoaji wa ajira katika Wizara hii kwa upande wa Zanzibar usijielekeze katika kwenye kikosi cha Jeshi la Kujenga Uchumu (JKU)?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Mkokotoni kilichoko Unguja?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Makazi ya askari yamekuwa ya zamani pia mengine yamekuwa mabovu sana, mfano nyumba za Ziwani Zanzibar, Wete, Pemba na Chakechake Pemba hazikaliki kabisa.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia marekebisho nyumba hizo?
(b) Je, ni gharama gani Serikali itatumia kwa marekebisho ya nyumba hizo?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Wafanyabiashara wanaotoa bidhaa kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara hutozwa kodi Zanzibar na wanapofika Tanzania Bara hutozwa kodi tena; vilevile, wafanyabiashara wanaotoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar, hutozwa kodi tena Zanzibar. Hali hii husababisha wafanyabiashara kushindwa kuendelea na biashara kwani wanatozwa kodi mara mbili:-
(a) Je, Serikali inatambua uwepo wa utaratibu wa kutozwa kodi mara mbili kwa wafanyabiashara?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi na wa kudumu kutatua suala la wafanyabiashara kutozwa kodi mara mbili?
MHE. MATTAR ALI SALUM Aliuliza:-
Kuna malalamiko makubwa kwa upande wa Zanzibar kuhusu idadi ndogo ya wanafunzi wanaopata Mkopo wa Elimu ya Juu jambo ambalo linapunguza idadi ya wataalamu kwa upande wa Zanzibar, hivyo kuingia katika soko la ajira katika Afrika ya Mashariki na Kati na kuijenga nchi yetu kwa ujumla.
(a) Je, Serikali haioni kuwa Bodi ya Mfuko wa Elimu ya Juu inatakiwa kutenga asilimia maalum kwa wanafunzi kutoka Tanzania Zanzibar?
(b) Je, bajeti iliyotengwa kwa mwaka huo wa 2015/2016 ni kiasi gani?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Tatizo la makazi kwa wanajeshi wetu ni kubwa kiasi kwamba maaskari wetu kupata usumbufu na kuathiri utendaji kazi wao.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za makazi kwa wanajeshi wa upande wa Unguja?
(b) Je, ni nyumba ngapi Serikali imepanga kujenga Zanzibar?
(c) Je, ni lini ujenzi wa nyumba kwa upande wa Zanzibar utaanza?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Jeshi la Polisi lina kazi kubwa ya kulinda usalama wa raia na mali zao, lakini cha kusikitisha ni kwamba askari wanaishi kwenye nyumba duni sana jambo ambalo linashusha hata hadhi zao hasa kwa upande wa Tanzania Zanzibar.
(i) Je, ni lini askari wetu watatengenezewa nyumba bora nao wajisikie kuwa Serikali yao inawajali?
(ii) Katika Makao Makuu ya Polisi pale Ziwani kuna majengo yaliyoachwa na wakoloni, je, kwa nini yasifanyiwe ukarabati mkubwa ili yaweze kutumiwa na askari wetu?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Wananchi wengi hapa nchini hasa wanawake hutumia vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu. Pamoja na jitihada za Serikali kuzuia bidhaa hizo lakini bado vinaingizwa nchini na kutumika.
(a) Je, Serikali ina mpango gani madhubuti wa kuzuia uingizwaji na utumiaji wa vipodozi hivi?
(b) Je, Serikali inaweza kutumia fedha kiasi gani kuzuia bidhaa hiyo kuingia nchini?
(c) Je, adhabu gani inatolewa kwa yeyote atakayekamatwa akiingiza nchini vipodozi visivyofaa kwa matumizi?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Usafiri wa kutumia bandari ni usafiri muhimu sana na ni wa lazima kwa watu wanaotoka Tanzania Bara kwenda Unguja na Pemba; na zipo kampuni zinazotoa huduma ya usafirishaji lakini hazitoshelezi katika kutoa huduma hiyo muhimu.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kununua meli ili kukidhi mahitaji ya usafirishaji wa watu wetu?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Uvuvi wa Bahari Kuu unaingiza kipato kikubwa sana na unaweza ukachangia katika bajeti ya nchi yetu:-
(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kununua meli za uvuvi?
(b) Je, Serikali imefikia wapi katika ujenzi wa Bandari ya Uvuvi nchini?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Polisi wanapowakamata watuhumiwa baadhi wanawaweka ndani kwa saa 24 na wengine zaidi ya saa 24.
• Je, ni makosa yapi mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani zaidi ya masaa 24?
• Je, ni makosa yapi ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-

Jeshi la Polisi lipo kwa mujibu wa sheria na hupaswa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi. Jeshi la Polisi linapowakamata baadhi ya watu huamuru wawekwe ndani zaidi ya saa 24 na kusababisha usumbufu mkubwa:-

Je, ni kesi zipi mtuhumiwa anapaswa kuwekwa ndani chini ya saa 24.
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-

Miongoni mwa kero za Muungano ni wananchi wa Zanzibar waletapo magari yao Tanzania Bara kutoruhusiwa kutembea mpaka yabadilishwe namba, wakati magari yanayotoka Bara yafikapo Zanzibar yanaruhusiwa kutembea kwa muda wote bila ya bughudha yoyote:-

(a) Je, Serikali inalifahamu suala hili?

(b) Kama ndiyo, je, Serikali ina mpango gani madhubuti wa kutatua suala hili ili Watanzania waendelee kufaidi matunda ya Muungano?
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-

Kampuni ya Azam Marine ambayo inafanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia boti kupitia baharini, huuza tiketi kwa abiria kwa ajili ya safari lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo huwa haitumiki na hivyo kusababisha hasara kwa abiria pamoja na usumbufu;-

(a) Je, Serikali inalijua hilo?

(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo hilo?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's