Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Primary Questions
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Mradi wa Maji wa Kijiji cha Manzase ulishalipiwa nusu ya gharama za mradi na Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Nne.
(a) Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina Mpango gani kuukamilisha ili wananchi wa Kijiji hicho wapate huduma ya maji safi na salama;
(b) Kijiji cha Chinoje kilipata Mradi wa World Bank na kuchimbwa visima 10 lakini maji hayakupatikana. Je, Serikali ina Mpango gani?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Jimbo la Mtera katika Kijiji cha Mvumi-Misheni aliahidi kutujengea barabara ya lami kutoka Mlowa Barabarani hadi Mvumi-Misheni kwenye Hospitali Teule ya Wilaya ya Chamwino. Pia Rais wa Awamu ya Tano katika kampeni zake alipofika Mvumi-Misheni alisisitiza kuwa barabara hiyo itajengwa haraka iwezekanavyo. Je, ujenzi huo utaanza lini?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Upo mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mpwayungu kwa jina maarufu Mgangalenga wa muda mrefu na Serikali imegharamia fedha nyingi sana.
Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huo ili wananchi waweze kunufaika nao?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Jimbo la Mtera katika kijiji cha Mvumi Misheni aliahidi kutujengea barabara ya lami kutoka Mlowa barabarani hadi Mvumi Misheni kwenye Hospital Teule ya Wilaya ya Chamwino. Pia Rais wa Awamu ya Tano katika kampeni zake alipofika Mvumi Misheni alisisitiza kuwa barabara hiyo itajengwa haraka iwezekanavyo.
Je, ujenzi huo utaanza lini?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Serikali iliunda chombo kinachosimamia barabara za Vijijini na Mijini kinachoitwa TARURA:-
Je, chombo hicho kitaanza lini kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwani barabara hizi ni mbaya sana hasa wakati wa masika?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani juu ya wanyama waharibifu hususan tembo ambao wamesambaa hovyo katika Jimbo la Mtera na kufanya uharibifu mkubwa pamoja na kuua watu?
MHE. OMARY A. BADWEL (K.n.y. MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE) aliuliza:-
Je, ni lini barabara ya kutoka Mpunguzi kupitia Nagula, Mpwajungu, Ituzi hadi Ilangali itapandishwa hadhi kuwa ya Mkoa ambayo itasimamiwa na Mkoa kwa maana ya TANROADS?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-

Wakazi wa Kitongoji cha Mafulungu kilichopo katika Kijiji cha Ilangali, Kata ya Manda wanajishuhgulisha na uchimbaji wa madini.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha wakazi hao ili shughuli zao za uchimbaji ziwe za ufanisi na zenye tija?
MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. LIVINGSTON J. LUSINDE) aliuliza:-

Kwa kuwa Serikali imehamia Dodoma, je, kwa nini Serikali isijenge Maktaba yenye kumbukumbu za kazi za Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo pia itakuwa sehemu ya utalii kwa watu wa ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-

Je, ni lini barabara ya Mvumi Mission itajengwa kwa kiwango cha lami?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kituo kikubwa cha polisi katika Jimbo la Mtera hususani katika Kijiji cha Mvumi Misheni ili kukabiliana na wimbi kubwa la uhalifu katika Jimbo la Mtera?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's