Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Primary Questions
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-
Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ni sehemu ya ghala la chakula la Taifa katika mikoa mitano (5) inayolima chakula kwa wingi nchini Tanzania; lakini kikwazo kikubwa ni usafirishaji wa mazao kufikia masoko ya nje ya Wilaya; Halmashauri imeomba ongezeko la bajeti ya barabara kufikia shilingi bilioni 7,969,000 ili kuweza kukarabati barabara zote muhimu na kuwezesha wakulima kusafirisha mazao yao kwa urahisi na hatimaye kuongeza kipato cha Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe:-
Je, Serikali ipo tayari kukubali ombi la Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe la kuongeza fedha katika bajeti ya 2016/2017?
MHE. EDWARD F. MWALONGO (K.n.y. MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA) aliuliza:-
Shule ya Sekondari ya Ndembela Wilayani Rungwe awali ilijengwa kwa nguvu za wananchi na baadaye Kanisa la Waadventista Wasabato liliingia kama wabia na kuiendeleza na hatimaye kuiendesha shule hiyo ikiwa na majengo yaliyokamilika. Baada ya wananchi kuihitaji shule yao, Kanisa limekubali kuirejesha kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa fidia ya Sh.947,862,000/= Halmashauri imeomba Wizara ya Elimu isaidie kulipa fidia hiyo:-
Je, ni lini Serikali itasaidia kurejesha shule hiyo mikononi mwa wananchi kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:-
Wakulima wa chai wa Wilaya ya Rungwe wanauza majani ya chai kati ya shilingi 230 hadi 240 kwa kilo, wakati wakulima wa Njombe wanauza majani ya chai kwa shilingi 500 kwa kilo huku kukiwa na Bodi moja na ni nchi moja.
Je, kwa nini wakulima wa chai Wilaya ya Rungwe wanalazimishwa kuuza majani mabichi ya chai kwa bei ndogo kuliko wakulima wa chai wa Wilaya za Njombe na Lushoto?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Kampuni ya Highland Estate Mbarali na wananchi wanaolizunguka shamba hilo kwa kuwa mwekezaji amekuwa akipora ardhi kwa wananchi na kusababisha uvunjifu wa amani kwa muda mrefu sasa?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-
(a) Ranchi ya NARCO Mbarali ilianzishwa kwa ajili ya mifugo; Je, ni kwa nini eneo hilo sasa linatumika kwa kilimo?
(b) Migogoro ya wakulima na wafugaji Mbarali imekuwa ni mingi; je, kwa nini Serikali isitoe eneo la Ranchi ya NARCO Mbarali ili litumike kwa ajili ya malisho ya mifugo?
MHE. AIDA J. KHENAN (k.n.y MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA) aliuliza
(a) Je, kuna sheria yoyote ya nchi inayomruhusu askari polisi kumkatamata mtuhumiwa, kumpiga na kumtesa kabla hajajua kosa lake na kabla ya kufikishwa katika Kituo cha Polisi?
(b) Je, Serikali inachukua hatua zipi za kuhakikisha kuwa askari wanaofanya vitendo kama hivyo wanawajibishwa kwa mujibu wa sheria za nchi?
(c) Je, mpaka sasa ni askari wangapi wameshachukuliwa hatua za kisheria kutokana na makosa ya kujichukulia hatua mkononi?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-
Je, ni lini ujenzi unaoendelea katika Vituo vya Afya Ikuti, Wilayani Rungwe na Ipinda Wilayani Kyela utakamilika ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kupata huduma kwa wakati?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-
Wakati ujenzi wa barabara muhimu ya Ipinda – Matema ukiendelea.
Je, ni lini wananchi, taasisi kama makanisa na ofisi za vijiji katika vijiji vya Matema, Katusyo, Mababu, Ngyekye, Katela na Ngeleka ambao hawajabomoa majengo yao kwa sababu hawajafidiwa fidia zao ambayo kimsingi ni haki yao na kupisha ujenzi unaoendelea wa barabara hii muhimu sana katika maendeleo na uchumi wa Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya zitalipwa fidia hizo?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya mchepuo ya Mlima Nyoka - Songwe yenye urefu wa kilometa 48.9 utaanza baada ya ya usanifu na upembuzi yakinifu kukamilika?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Kwa mujibu wa GN. No. 222 na 223 ya mwaka 1972 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2002, Wazee wa Mabaraza ya Mahakama wanateuliwa na vikao vya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Kamati za Maadili za Mahakimu zipo chini ya Uenyekiti wa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya:-

Je, ni lini Mahakama itaacha kuingiliwa na siasa?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Michezo mingi ikiwemo mpira wa miguu inapata ufadhili sana hapa nchini kupitia kampuni mbalimbali binafsi na za Kiserikali:-

Je, ni lini Serikali itahakikisha ufadhili unapatikana kwenye michezo inayohusu wanawake hususan michezo ya ngumi kwa wanawake?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Katika Bajeti ya Mwaka 2017/2018 Serikali iliondoa kodi kwenye taulo za kike (pads) jambo ambalo ni muhimu sana kwa maisha ya Wanawake na Wasichana mpaka sasa ni mwaka mmoja tangu kodi hizo ziondolewe lakini bei ya taulo za kike haijashuka licha ya kuondolewa kwa kodi hizo Nchi nzima.

Je, ni lini Serikali itasimamia kwa ukamilifu suala hilo ili bei za taulo za kike zishuke na kusaidia afya za Wanawake hususani Wasichana?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Katika kujenga Tanzania ya viwanda, Serikali imekuwa na mikakati ya muda mrefu.

Je, ule mkakati wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI wa kujenga viwanda 100 kwa kila Mkoa ni sehemu ya mkakati na umeainishwa kwenye waraka gani wa Serikali ili kuwapa wananchi rejea ya pamoja ya kitaifa?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:-

Serikali imezuia kampuni binafsi kununua kokoa katika Wilaya za Kyela na Rungwe kwa msimu huu na Vyama vya Ushirika havina uwezo wa kununua kokoa hizo kwa wananchi:-

Je, ni lini Serikali itaruhusu tena kampuni binafsi kuendelea kununua kokoa?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka wakaguzi ili kuhakiki thamani ya fedha ya Shilingi bilioni 15 zilizotolewa na Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya mradi wa maji wa Masukulu ambao unaonekana kujengwa chini ya kiwango?
MHE. SOPHIA H. MWAKANGENDA aliuliza:-

Je, ni kwa nini wananchi wa Wilaya ya Rungwe wanalazimishwa kuuza chai na maziwa kwa mnunuzi mmoja hali inayosababisha mnunuzi kupanga bei kitu ambacho ni kinyume na Sera ya Ushindani wa Biashara?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Je, ni lini barabara ya Kiloba – Njugilo yenye urefu wa kilometa 7 itajengwa ili kurahisisha mawasiliano ya wananchi na wanafunzi wanaokwenda Kata ya Masukulu – Rungwe?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza: -

Je, ni lini mgodi wa makaa ya mawe Kiwira utapata Mwekezaji mpya na kulipa mafao ya waliokuwa wafanyakazi wa mgodi huo?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Wapimaji wa Ardhi katika Mji wa Tukuyu Wilayani Rungwe ili kupunguza migogoro ya ardhi?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya kilimo kuwa kipaumbele cha kwanza cha Taifa kwa kupunguza bei ya mbolea?
MHE. AIDA J. KHENANI K.n.y. MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaongeza fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa REA III katika Wilaya za Busokelo na Rungwe?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itabadili majina ya kigeni kuwa ya Kitanzania kwenye rasilimali za Taifa ikiwemo Mlima Livingstone na Ziwa Victoria?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itahakikisha Watanzania wanaofanya kazi kwenye Kampuni za Kichina wanalipwa vizuri kwa mujibu wa sheria?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: -

Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Je, kwa nini Serikali inaajiri kwa kigezo cha mwaka wa kumaliza chuo na kupitia mafunzo ya jeshi?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itashughulikia kuboresha ujira wa madereva wa magari ya IT?

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Je, Serikali ina kauli gani kuhusu mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa kuwa mfumo unawaacha nje vijana wengi kwa kukosa sifa?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaharakisha na kumaliza upembuzi yakinifu kwa ajili ya mradi wa maji katika vijiji 46 Wilaya ya Rungwe?
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuongeza bei ya chai Wilayani Rungwe kutoka shilingi 340 hadi shilingi 700 kwa kilo hasa ikizingatiwa kupanda kwa gharama za mbolea na madawa?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's