Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Dr. Jasmine Tiisekwa Bunga

Primary Questions
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-
Chuo Kikuu cha Mzumbe ni chuo kikongwe chenye historia tangu mwaka 1953 kipindi cha ukoloni na mwaka 1972 kupandishwa hadhi kuwa Chuo cha Uongozi wa Maendeleo (IDM) kikiwa na miundombinu ya kukidhi wanafunzi wasiozidi 1,000. Kwa sasa chuo hiki kina jumla ya wanafunzi 11,282 ambapo idadi hii ni sawa na ongezeko la 874.3% wakati hali ya majengo na miundombinu kwa kiasi kikubwa bado ni ile ile ya mwaka 1972:-
Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga miundombinu mipya ikiwemo madarasa, mabweni, ofisi za Wahadhiri, jengo la utawala na kadhalika ili kukidhi mahitaji ya ongezeko kubwa la wanafunzi na Wahadhiri waliopo na watakaokuja na kukifanya chuo hiki chenye historia kubwa kiwe na taswira ya chuo cha kisasa na hadhi ya kimataifa?
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-
Hospitali ya Mkoa wa Morogoro pamoja na changamoto zinazoikabili za kuwa na wagonjwa wengi, kukosekana kwa Hospitali za Wilaya, kupokea majeruhi wa ajali mbalimbali lakini hadi sasa hospitali hiyo inatumia X-ray za zamani ambazo ni chakavu hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa.
Je, ni lini Serikali itapeleka x-ray ya kisasa (Digital X- ray) ili kuondokana na adha kubwa wanayopata wagonjwa?
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-
Milima ya Uluguru ni chanzo kikubwa sana cha maji katika mito na vijito vingi ambavyo husaidia kwa kiwango kikubwa upatikanaji wa maji safi na salama katika Mkoa wa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam. Hata hivyo, kutokana na uharibifu wa mazingira uliosababishwa na ujenzi holela, kilimo na ufugaji, mito hiyo imeanza kukauka hivyo kusababisha adha kubwa ya upatikanaji wa maji kwa wananchi:-
Je, Serikali ina mipango gani ya kimkakati ya kuilinda milima hiyo isiendelee kuharibiwa na kuhakikisha miti iliyokatwa inapandwa mingine ili kuhifadhi vyanzo vya maji?
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-
Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi sana vya utalii ambavyo vikitumika vizuri vinaweza kuchangia pato la Taifa na wananchi kwa ujumla; moja kati ya vivutio hivyo ni pamoja na Mbunga za Hifadhi ya Wanyama Mikumi ambayo inaongeza mapato mengi, lakini mbuga hizo hazina hoteli nzuri za kitalii zenye kukidhi viwango vya kimataifa, kutokana na kuungua kwa Hoteli ya Kitalii ya Mikumi.
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga hoteli kubwa za kitalii ndani ya Mbuga ya Mikumi ili kuvutia watalii wengi?
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-

Kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi dhidi ya Mamlaka za Maji Safi katika Halmashauri mbalimbali kwa kuwapatia wananchi bili kubwa za maji ambazo haziendani na uhalisia:-

Je, ni lini Serikali itaanzisha utaratibu wa kulipia maji kadri utumiavyo katika utoaji wa huduma hiyo kama ilivyo kwenye umeme?
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-

Barabara zinazotoka Kidiwa hadi Tandali, Daraja la Mgeta hadi Likuyu, Visomolo hadi Lusungi na Langali SACCOS hadi Shule ya Sekondari Langali Tarafa ya Mgeta Wilayani Mvomero zimejengwa kwa nguvu za wananchi, lakini bado hazipitiki kutokana na vikwazo vya miundombinu na madaraja:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hizo ili kuondoa adha wanazopata wananchi?
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-

Baadhi ya watoto wakubwa wenye uwezo wameamua kuwatelekeza wazazi wao pasipo kuwapa matunzo wanayostahili:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawajibisha watoto waliotelekeza wazazi wao na kuhakikisha wanatoa matunzo stahili?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's