Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Primary Questions
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Serikali kwa miaka mingi imekuwa na mpango wa kujenga Hospitali za Rufaa za Kanda; na tayari Kanda zote zina hospitali hizo isipokuwa Kanda ya Kusini tu:-

(a) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga hospitali hiyo ya Kanda ya Kusini ambapo tayari eneo la Mitengo Mikindani limetengwa kwa zaidi ya miaka saba na hakuna kinachoendelea?

(b) Je, ni Serikali haioni kama hawatendei haki wananchi wa maeneo ya Kanda ya Kusini kama wananchi wa maeneo mengine?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Mafuriko yanayotokea Mtwara Mjini kila mwaka hasa katika Kata ya Shangani, Cuono, Magomeni na Ufukoni yanasababishwa namiundombinu mibovu ambayo imejengwa chini ya kiwango katika maeneo mengi ya Mji wa Mtwara:-
(a) Je, Serikali iko tayari sasa kujenga upya mitaro, madaraja pamoja na miundombinu mingine ili maji yaweze kusafiri kuelekea baharini wakati wa masika?
(b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara ya Mikindani - Lwelu ufukweni mwa bahari kwa kiwango cha lami ikizingatiwa kuwa barabara hiyo iko ndani ya Manispaa?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Miundombinu ya maji Mtwara na mikoa yote ya Kusini mwa Tanzania ni hafifu na wakazi wengi wa miji ya Kusini na vijijini hawapati maji safi na salama.
Je, Serikali iko tayari kujenga bomba la kuvuta maji toka Mto Ruvuma ambalo limekuwa likizungumzwa kwa muda mrefu bila mafanikio?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa Mwanza alipiga marufuku na kuziagiza mamlaka zinazohusika kuacha kuwasumbua wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga:-
Je, Serikali inatekeleza agizo hilo kwa kiwango gani?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA Aliuliza:-
Gesi inayochakatwa Mtwara huweza kuzalisha viwanda vidogo vidogo ikiwemo mbolea na kwa miaka mingi wananchi wa Mtwara wamekosa fursa ya ajira ukilinganisha na maeneo mengine ya Tanzania kama vile Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na kadhalika.
Je, ni lini Serikali itasitisha usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi ili wana Mtwara waweze kunufaika na ajira zinazotokana na uchakataji wa gesi hiyo asilia kufanyika Mtwara na Seriakli kujenga viwanda vitokanavyo na gesi Mtwara?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Mwaka 2012/2013 Serikali ilichukua ardhi ya wananchi wa Mtwara Mjini eneo la Mji Mwema na Tangira. Aidha, Serikali imewazuia wananchi hao kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo hayo. Serikali iliahidi kuwalipa wananchi hao fidia lakini hadi sasa fidia hiyo haijalipwa.
Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi wao?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Manispaa ya Mtwara Mikindani ina migogoro mikubwa ya ardhi inayokaribia kusababisha uvunjifu wa amani:-
Je, Serikali ipo tayari hivi sasa kutatua migogoro hiyo?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Je, kuvunjwa kwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kuna faida gani kwa wakazi wa Dodoma?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Bandari ya Mtwara ni Bandari yenye kina kirefu Afrika Mashariki na Kati na Serikali kwa makusudi imeamua kuitupa na kujenga Bandari katika maeneo mengine ya nchi tena kwa gharama kubwa sana:-
Je, Serikali ipo tayari kukiri makosa na kuiboresha Bandari ya Mtwara ili korosho zote zisafirishwe kupitia Bandari hiyo kwa lengo la kupunguza msongamano katika Bandari ya Dar es Salaam?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Je, kwa nini Serikali haisemi ukweli Bungeni juu ya fidia kwa wananchi wa Mtwara Mjini?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Serikali imeanzisha utaratibu wa kutoa elimu bure na kuanza kutekeleza utaratibu huo kwa kupeleka fedha shuleni kidogo kidogo kulingana na idadi ya wanafunzi husika tangu Oktoba 25, 2015:-
(a) Je, Serikali inafahamu kwamba shule nyingi za msingi na za sekondari nchini zikiwemo za Mtwara Mjini zilikuwa na madeni mengi ya wazabuni na steshenari?
(b) Je, Serikali inaweza kueleza kuwa madeni hayo yatalipwa kwa utaratibu upi ikiwa fedha zinazotolewa ni kidogo kwa uwiano wa mwezi kwa mwaka husika?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Je, kwa nini Serikali haitaki kukarabati Uwanja wa Ndege Mtwara?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Zao la Korosho pamoja na kuingiza mapato makubwa Serikalini bado lina changamoto nyingi sana katika uuzaji wake kwa upande wa Wakulima:-

Je, Serikali ipo tayari kuondoa changamoto hizo ili kuleta tija kwa Wakulima?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itavunja Bodi za Wahandisi kutokana na kauli ya Mheshimiwa Rais?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Je, Serikali inahakikishaje amani na utulivu vinakuwepo katika chaguzi mbalimbali nchini?
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi kubwa na ngumu sana hasa Mtwara Mjini na maeneo mengine ya nchi yetu.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwalipa mishahara kama ilivyo kwa Watendaji wa Vijiji na Mitaa?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

Member of the Parliament

View All MP's