Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Haroon Mulla Pirmohamed

Primary Questions
MHE. HAROON M. PIRMOHAMED aliuliza:-
Katika GN. Na. 28 ya mwaka 2008 inawataka wananchi wanaoishi katika vijiji 21 vilivyopo katika Jimbo la Mbarali, Wilaya ya Mbarali, Mkoani Mbeya wahame ili kupisha Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ingawa wananchi katika vijiji hivyo wameishi katika maeneo hayo tangu enzi za mababu zao:-
Je, ni lini Serikali itafuta GN. Na. 28 ya mwaka 2008 ili wananchi katika vijiji hivyo waweze kuishi bila kubughudhiwa pamoja na kuendelea na shughuli zao za kilimo na ufugaji?
MHE. ORAN M. NJEZA (K. n. y MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:-
Mji Mdogo wa Rujewa ni kitovu cha shughuli za biashara na Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali na kwa bahati mbaya barabara nyingi za mji huo hazipitiki kutokana na ubovu. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami.
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kwa wananchi wa Mbarali?
MHE. HAROON M. PIRMOHAMED aliuliza:-
Barabara ya Rujewa – Madibira ni tegemeo na ni kiungo muhimu kati ya Rujewa – Madibira na Madibira – Mafinga na Serikali imekuwa ikitoa ahadi kwa muda mrefu kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami. Je, ni lini sasa barabara hiyo itaanza kujengwa?
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itamaliza kujenga Skimu za Umwagiliaji za Ipatagwa, Kongoro/ Mswiswi, Motombaya na ujenzi wa Skimu mpya ya Mhwela mpaka Kilambo pamoja na ujenzi wa Banio la Igumbilo, Kata ya Chimala ambalo lilibomolewa na maji mwaka 2016?
MHE. ORAN M. NJEZA (K.n.y. MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itafanyia ukarabati barabara za Mahongole – Kilambo kilometa 20, Igurusi – Utengule kilometa 22, Chimala – Kapunga kilometa 25 na Mlangali – Ukwavila kilometa 23?
MHE. DKT. TULIA ACKSON (K.n.y HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka maji maeneo katika maeneo ya Kata za Mahongele katika vijiji (6), Kata ya Mwatenga vijiji (4), Kata ya Kongoro/Mswiswi vijiji (2), Kata ya Utengule - Usangu vijiji (6), Kata ya Luhanga vijiji (4), Kata ya Itambo vijiji (4), Kata ya Chimala vijiji (7), Kata ya Ihahi vijiji (3), Kata ya Imalilo – Songwe vijiji (5), Kata ya Igaua vijiji (5), Kata ya Miyombweni vijiji (5), Kata ya Mapogoro vijiji (9) na Mji wa Rujewa?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's