Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Primary Questions
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-
Kwa muda mrefu wananchi wa Busokelo wamekuwa wakikumbana na adha kubwa ya ubovu wa barabara ya Katumba - Mbando - Tukuyu yenye urefu wa kilometa 82 inayoanzia Katumba (RDC) kupitia Mpombo, Kandete, Isange, Lwangwa, Mbwambo (BDC) hadi Tukuyu (RDC) na barabara hii imekuwa kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami kwa muda mrefu na Mkandarasi yuko eneo la ujenzi wa kipande cha kilometa kumi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha barabara hiyo kwa kujenga sehemu iliyobaki yenye kilomita 72?
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-
Wananchi wa Bonde la Mwakaleli, Kata za Kandete, Isange na Luteba wanaoishi kando ya Hifadhi ya TANAPA wamekuwa wakinyanyaswa sana na watumishi wa TANAPA kwa kisingizio kwamba wamevamia Hifadhi wakati TANAPA ndio waliovamia makazi ya wananchi kwa kuweka mipaka mipya tofauti na ile ya zamani hali inayofanya baadhi ya shule na taasisi zingine kuonekana kuwa ndani ya Hifadhi ya TANAPA kwa sasa:-
Je, ni lini Serikali itarudisha mipaka ya zamani ili wananchi wasiendelee kuishi kwa wasiwasi, lakini pia waendelee na shughuli za kilimo kama ilivyokuwa zamani?
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-
Wananchi wa Jimbo la Busokelo hasa katika Kata za Kandete, Isange, Lutebe Lwangwa, Mpata, Kabula, Mpombo, Lufilyo Kambasegela, Ntaba, Lupata, Itete, na Kisegese wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji safi na salama; na kuna maeneo mengi ambayo mabomba uyamepita lakini maji hayatoki kutokana na kukosekana kwa matenki ya maj:-
(a) Je, ni lini Serikali itatatua kero hiyo ya maji kwa kujenga matenki ya maji kwenye Kata hizo?
(b) Mji wa Lwangwa ni Makao Makuu ya Halmashauri mpya ya Busokelo na kuna ongezeko kubwa la watu ukilinganisha na miundombinu ya maji iliyopo; je, Serikali ina mpango gani wa kujenga miundombinu mipya ya uzalilshaji wa maji kwenye eneo hilo jipya la mipango miji?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
Serikali imekuwa ikiahidi kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya ili kuwaondolea kero wananchi wanaosafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya na wengine kupoteza maisha wakiwa njiani:-
Je, ni lini Serikali itatekeleza mpango huo wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji, Kituo cha Afya kwa kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
(a) Je, Serikali itakubali kujenga Hospitali ya Wilaya ya Busokelo hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wametoa eneo tayari na wako tayari kushirikiana na Serikali?
(b) Je, kama Serikali inakubali, ni lini kazi hiyo itaanza?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
Halmashauri ya Busokelo ina changamoto za miundombinu ya barabara ambayo hairidhishi, na ukizingatia kuwa wananchi wake wanategemea zaidi shughuli za kilimo na usafirishaji wa gesi asilia ya carbondioxide.
(a) Je, ni lini Serikali itajenga barabara inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Njombe kupitia Mwakaleli, kata za Kandete na Luteba?
(b) Je, ni lini Serikali itajenga barabara inayounganisha Jimbo la Busekelo (kijiji cha Kilimansanga) na Jimbo la Rungwe (kijiji cha Suma)?
(c) Vyanzo vya Halmashauri haviwezi kujenga barabara zote na hivyo kulazimika kuomba msaada TANROADS; je, ni lini maombi ya Halmashauri ya Busekelo, kuhusu kupandishwa hadhi ya barabara zaidi ya tano tulizoomba ili ziwe chini ya TANROADS yatajibiwa?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE Aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itayakubali maombi ya wananchi wa Halmashauri ya Busokelo ya kuifanya Halmashauri hiyo iwe Wilaya?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
Ajira kwa sasa ni tatizo hapa nchini hasa kwa walimu wa sanaa.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuajiri katika sekta mbalimbali?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
Tunatambua juhudi za Serikali za kujenga Chuo cha Kilimo na Mifugo katika Kata ya Lufyilo.
Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa bwalo la nyumba za walimu ili chuo hicho kianze kutoa huduma kwa wananchi, hasa ikizingatiwa kuwa majengo ya madarasa yalishakamilika?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
Hapa nchini kumekuwepo na ukuaji na utumiaji wa mifumo mingi mipya ya teknolojia kwa ukusanyaji wa kodi na malipo mengine kwa njia ya mtandao (electronic):-
(a) Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na wizi wa kimtandao kwa wananchi?
(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuundwa kwa Bodi ya wana TEHAMA nchini ili kuwa na udhibiti na ufanisi wa watumiaji wa mitandao nchini wanataaluma wa TEHAMA waweze kuwa na Bodi hiyo?
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y MHE. FREDY A. MWAKIBETE) aliuliza:-
Tanzania imebarikiwa kuwa na madini mbalimbali na Jimbo la Busokelo pia limebarikiwa kuwa na madini hayo.
Je, ni lini Serikali itapeleka wawekezaji wa kiwanda cha marumaru katika Kata ya Lufilyo kwenye Mto Makalya?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
Busokelo ni miongoni mwa Halmashauri zinazozalisha maziwa ya ng’ombe kwa wingi ambapo kwa mwaka inazalisha zaidi ya lita milioni 50:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia kumalizia Kiwanda cha Maziwa kinachojengwa Kata ya Isange ili kunusuru maziwa mengi yanayoharibika kwa kukosa soko?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
Halmashauri ya Busokelo ina utajiri mkubwa wa madini na gesi asilia aina ya carbon dioxide:-
Je, ni lini Serikali itaenda kufanya utafiti wa kutosha kwenye Kata ya Lufilyo ambapo kuna madini aina ya marble (marumaru)?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-

Halmashauri ya Busokelo ina maporomoko ya maji (waterfalls) maeneo mbalimbali na jotoardhi (geothermal):-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutumia maporomoko hayo ya maji (waterfalls) na jotoardhi (geothermal) kuweza kuzalisha umeme ili kupunguza changamoto ya umeme nchini?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-

Wananchi wa Busokelo katika Kata ya Luteba walianza kutengeneza barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya na Njombe kupitia Mlima ya safu za Livingstone:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kuunga mkono juhudi za wananchi hao?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-

Wananchi wa Kata za Mpombo, Kandete, Isange na Luteba pamoja na Kata za Kabula, Lwanga na Lupata wanalima zao la chai kwa wingi lakini bei ya zao hilo ipo chini:-

Je, ni lini Serikali itatafuta soko la uhakika la zao la Chai ambalo litasababisha kupanda kwa bei kuliko bei ya sasa ya Shilingi 315 kwa kilo?
MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-

Katika eneo linalopatikana gesi aina ya carbondioxide (CO2) kwenye Jimbo la Busekelo, Kijiji cha Mpata kuna visima ambavyo ni hatari kwa binadamu na viumbe hai wengine kwani huwa wanakufa wakivuta hewa ya sehemu hiyo:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kunusuru maisha ya binadamu na viumbe katika eneo hilo?
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE Aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa Daraja la Mto Mbaka linalounganisha Jimbo la Busokelo na Rungwe litakamilika?
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE Aliuliza: -

Je, ni kwa kiwango gani Serikali inajiridhisha kuwa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu imetolewa kwa wanafunzi walengwa?
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Umeme wa Maji kutoka Mto Rumakali katika Kata ya Lufilyo utaanza?
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa wananchi maeneo ya Hifadhi ya Kitulo ambayo hayatumiki ili wayatumie kulisha mifugo yao hususani eneo la Kwipanya?
MHE. ATUPELE F. MWAKIBE aliuliza: -

Je, lini Mkataba wa Ujenzi wa Barabara ya Katumba – Mbambo hadi Tukuyu utasainiwa kwa kuwa Mkandarasi alishapatikana?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

Member of the Parliament

View All MP's