Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Dr. Elly Marko Macha

Primary Questions
MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. DKT. ELLY M. MACHA) aliuliza:-
Kufuatia Mpango wa Serikali wa utoaji wa elimu bure kuanzia Elimu ya Msingi hadi Sekondari na kwamba, watu wenye Ulemavu wanakabiliwa na umasikini uliokithiri na hivyo kushindwa kumudu gharama za elimu:-
(a) Je, Serikali iko tayari kutoa elimu bure kwa wanafunzi wenye ulemavu kwa ngazi ya Kidato cha Tano na Sita?
(b) Je, Serikali inaweza kulihakikishia Bunge hili kwamba itaweka utaratibu mzuri wa usafiri na huduma nyingine muhimu za kuwawezesha wanafunzi wenye ulemavu kupata elimu katika shule wanazopangiwa?
(c) Je, Serikali inaweza kulithibitishia Bunge hili kwamba wanafunzi wenye ulemavu wanaoingia Vyuo Vikuu watapewa kipaumbele katika kupata mikopo bila usumbufu wowote?
MHE. DKT. ELLY M. MACHA aliuliza:-
Elimu kwa watoto wenye ulemavu hupatikana kwa vikwazo na matatizo mengi kiasi kwamba wengi huanza shule katika umri mkubwa ukilinganisha na watoto wasio na ulemavu:-
(a) Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuongeza umri wa kustaafu kwa lazima kuwa miaka 65 kwa watu wenye ulemavu?
(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa upendeleo maalum wa ajira kwa watu wenye ulemavu katika Wizara na Taasisi zake pale ambapo mtu mwenye ulemavu atakuwa na sifa stahiki wakati wa zoezi la ajira?
MHE. DKT. ELLY M. MACHA aliuliza:-
Katika miaka ya 60 na 90, Serikali yetu kwa ufadhili wa nchi rafiki kama Norway na Sweden ilijenga vyuo vya ufundi vilivyotoa mafunzo mbalimbali kwa watu wenye ulemavu hapa nchini kama vile Yombo - Dar es Salaam, Singida, Mtapika – Masasi, Masiwani – Tanga, Mbeya, Ruanzari – Tabora na Mwirongo-Mwanza; hivi sasa kati ya vyuo saba ni vyuo viwili tu vya Yombo na Singida ndiyo vinafanya kazi tena kwa kusuasua:-
(a) Je, ni sababu zipi zilizosababisha vyuo hivyo vitano vifungwe wakati kuna mahitaji makubwa ya watu wenye ulemavu kupata mafunzo ya ufundi?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua haraka vyuo hivyo vilivyofungwa ili viendelee kutoa mafunzo ya ufundi kwa watu wenye ulemavu?
(c) Ili kutoa fursa zaidi za mafunzo ya ufundi kwa watu wenye ulemavu, je, Serikali ina mkakati gani wa kujumuisha watu wenye ulemavu kwenye vyuo vyake vya VETA na FDC?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's