Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Flatei Gregory Massay

Primary Questions
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Kutokana na wizi wa mifugo uliokithiri katika Bonde la Yayeda Chini, Serikali ilianzisha kituo cha polisi na sasa kimeondolewa:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukirudisha kituo hicho ili wananchi wapate huduma za ulinzi wa mifugo na mali zao?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Barabara ya Mbulu – Hydom – Babati – Dongobeshi, imekuwa na miundombinu mibovu na haipitiki muda wote wa mwaka na kumekuwepo ahadi ya kutengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
Je, Serikali itatekeleza lini ahadi hiyo ambayo pia imetolewa na Mheshimiwa Rais wa awamu ya tano?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Serikali kupitia Benki ya Dunia ilianzisha mradi wa maji katika Miji ya Haydom, Masieda, Tumati Arri na Bwawa la Dongobesh lakini mpaka sasa mradi huo haujakamilika baada ya fedha kusitishwa:-
Je, Serikali imejipangaje kumaliza miradi hii ili wananchi wapate maji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika maeneo ya Tarafa za Jimbo la Mbulu za Manetadu, Tumatu Arri, Masieda na Yayeda chini?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka ruzuku katika Hospitali ya Haydom ambayo pia ni Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara ambayo inatumiwa na Mikoa ya Singida, Simiyu, Arusha pamoja na Jimbo la Meatu?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Hospitali ya KKKT Hydom ilipanda hadhi kuwa Hospitali ya Mkoa muda mrefu, sasa inahudumia Mikoa ya Manyara, Shinyanga, Singida, Arusha na Simiyu:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuipandisha hadhi ili iwe Hospitali ya Kanda kuiwezesha kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Wananchi wa Mji wa Haydom wamekuwa wakiomba Haydom iwe Mamlaka ya Mji Mdogo.
Je, ni lini Serikali itaupa Mji wa Haydom hadhi hiyo?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Wananchi wa Mbulu Vijijini hawana mawasiliano ya simu wala minara katika Kata za Tumati, Yaeda, Ampa, Gidhim na Gorati:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka minara katika Kata hizo ili kupata mawasiliano?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Serikali kupitia Mradi wa Vijijini kumi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia iliahidi kupeleka maji Maretadu, Labay, Gidmadoy, Qamtananat, Garbabi, Magana Juu na Qatabela:-
Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya utekelezaji wa ahadi hiyo?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Mradi wa Maji wa Hydom umechukua muda mrefu kumalizika na wananchi wanasubiri maji huku muda wa mkataba na mkandarasi ukiwa umeisha.
Je, kwa nini Serikali isimfukuze mkandarasi huyo?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Serikali ina mpango gani wa kuwalipa posho au mishahara Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji ili kurahisisha ufanisi wa shughuli zao?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya Simu katika Kata za Yayeda, Ampa Arr, Tumati, Gidilim Gorati, Endaagichan na Haydere katika Jimbo la Mbulu Vijijini ili wananchi waweze kuwasiliana?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Kutokana na sera ya Serikali kujenga vituo vya afya kila kata.
Je, ni lini Serikali itajenga vituo hivyo katika Kata za Maretadu, Maghangw, Endamilay, Dinamu, Geterer, Masieda na kupandisha hadhi Zahanati ya Hayderer kuwa Kituo cha Afya?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III.
Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Serikali iliahidi kuanzisha Baraza la Ardhi la Wilaya ya Mbulu. Aidha, wataalam wa Serikali walifika Mbulu na kukabidhiwa majengo kwa ajili ya Baraza hilo katika Mji wa Dongobesh na Mheshimiwa Mbunge akachangia shilingi milioni tatu za kuongeza miundombinu.

Je, ni lini Baraza la Ardhi la Wilaya ya Mbulu litaanzishwa?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Madiwani nchini wanafanya kazi kubwa sana.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea posho na mishahara au maslahi yao?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Wakulima wa vitunguu saumu wanayo changamoto ya soko la kuuzia zao hilo:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta soko la vitunguu saumu nje ya nchi?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Serikali aliahidi kupeleka umeme katika vijiji vyote vya Jimbo la Mbulu Vijijini kupitia REA III kwa sababu REA II haikufanya vizuri katika jimbo hilo:-

Je, vijiji vingapi vitafikiwa na umeme wa REA Awamu ya III?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Wananchi wa Hydom wameandaa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama kwa sababu Polisi wakikamata watuhumiwa huwapeleka Mbulu Mjini kilomita 86 ilipo Mahakama ya Wilaya:-

(a) Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Hydom?

(b) Je, Serikali haioni kuwa inapata hasara sana kupeleka Mahabusu Mbulu Mjini umbali wa kilomita 86 kutoka Hydom?
MHE. FLATEI G. MASSAY Aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Karatu – Dongobesh – Hydom hadi Singida iliyotengewa fedha katika bajeti iliyopita utaanza?
MHE. FLATEI G. MASSAY Aliuliza:-

Je, ni lini minara ya simu itajengwa katika Kata za Endahagichen – Ndamilay, Mewadan – Magong na Endaghadat – Qamtananat katika Jimbo la Mbulu Vijijini ambazo hazina mawasiliano ya simu?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Jimbo la Mbulu Vijijini ili vijana wapate ujuzi?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Mahakama Hydom katika Jimbo la Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbulu – Haydom – Singida kwa lami, ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais tangu mwaka 2015?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Ujazilizi katika Mkoa wa Manyara na Jimbo la Mbulu Vijijini ili kuwafikia wananchi wengi ambao hawakupitiwa na Mradi wa REA I, II na III?
MHE. FLATEI G. MASSAY Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka umeme katika Vijiji na Vitongoji vya Jimbo la Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, lini minara ya mawasiliano itajengwa katika Kata za Endanywish, Endagulda, Gidurdagaw, Yaeda Ampa, Hayeda na Endanilay?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti matukio ya ubakaji wa akina mama uliokithiri katika Jimbo la Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga mabwawa katika Jimbo la Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Geterer na Masieda?
MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kupeleka mbegu za mahindi kabla ya kipindi cha masika katika Jimbo la Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini minara ya simu itajengwa maeneo ya Endahagichang, Tumati Juu, Qalodaginwe, Aidurdagawa, Qamtananat na Migwa?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA katika Kata na Vijiji 23 vya Jimbo la Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Je Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea zaidi posho Madiwani na kuwalipa mishahara Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's