Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Hassan Selemani Kaunje

Primary Questions
MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
Jimbo la Lindi Mjini lina eneo la Bahari ya Hindi lenye urefu wa kilometa 112, lakini eneo hilo halina mchango wowote wa maana kwenye pato la Taifa na Manispaa ya Lindi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza eneo la bahari katika Manispaa ya Lindi?
MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015 - 2020, imeeleza juu ya uendelezaji wa utalii kwa Ukanda wa Kusini kama Program Maalum:-
Je, ni lini Serikali imepanga kuanza mpango huo maalum?
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:-
Kuna migogoro ya ardhi iliyosababishwa na upimaji na ugawaji wa ardhi kwa ajili ya makazi na ujenzi wa taasisi katika Kata ya Rasbura eneo la Mitwero.
Aidha, watumishi wa Idara ya Ardhi walijigawia ardhi kinyume na taratibu na kuiuza kwa manufaa yao. Pia wananchi wanalalamikia fidia na utwaaji wa maeneo makubwa tofauti na michoro iliyomo kwenye nyaraka zilizothibitishwa na Wizara kwa matumizi ya taasisi za umma au binafsi:-
Je, Serikali ipo tayari kufanya uchunguzi au uhakiki wa zoezi zima la upimaji na ugawaji wa viwanja katika eneo hilo?
MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 inasema kuwa idadi ya watu katika Jimbo la Lindi Mjini ni takribani 78,000, lakini takwimu za watu waliojiandikisha NIDA inafika 100,000 na sensa iliyofanywa kupitia Serikali za Mitaa inaonyesha kuwa wakazi wa Lindi Mjini ni zaidi ya 200,000 na Serikali inaendelea kupanga mipango yake ya maendeleo kwa kutumia takwimu za watu 78,000 hivyo kuathiri huduma stahiki za maendeleo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuangalia upya takwimu hizo ili wananchi wa Lindi Mjini wapelekewe huduma za maendeleo stahiki?
MHE. HASSANI S. KAUNJE aliuliza:-
Mradi wa Maji wa Ng’apa ambao upo Manispaa ya Lindi ulikusudiwa kuwahudumia wakazi wa Lindi Mjini tangu mwezi Mei, 2015, lakini mpaka sasa mradi huo haujakamilika. Je, ni lini mradi huo utakamilishwa?
MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
Hospitali ya Rufaa ya Sokoine Mkoani Lindi inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maji na ubovu wa vyoo katika wodi zake, pia watumishi wa hospitali hiyo wamekuwa na lugha na huduma duni zinazokera wateja.
Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto zinazoikabili hospitali hiyo?
MHE. HASSAN E. MASALA (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Ngongo - Ng’apa - Milola ambayo ipo chini ya TANROADS?
MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:-
Kuna mgogoro wa ardhi wa muda mrefu kati ya wananchi wa kijiji cha Mkwaya na mwekezaji Durbali:-
Je, ni lini mgogoro huo utapatiwa ufumbuzi?
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S.
KAUNJE) aliuliza:-
(a) Je, ni lini Serikali itadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge?
(b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/ mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?
MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
TANROADS ilifanya upanuzi wa Road Reserve tangu mwaka 2011 ambayo ilihusisha tathmini ya mali zilizopo kwenye maeneo husika:-
Je, ni lini wananchi wa Lindi watalipwa stahili zao?
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:-

(a) Je, ni lini Serikali itawadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge?

(b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's