Parliament of Tanzania

Do's and Don'ts

Mambo ya Kuzingatia wakati wa Kutembelea Bunge

Vikao vya Mikutano ya Bunge huanza saa 3:00 asubuhi na kwa kawaida huendelea hadi saa 7:00 mchana ambapo husitishwa. Wabunge hurejea tena saa 11:00 jioni na kikao huendelea hadi saa 1:45 usiku ambapo Bunge huairishwa mpaka siku inayofuata. Hivyo basi, wageni wote wanapaswa wawe wameketi katika maeneo husika kabla ya saa 2:45 asubuhi na saa 10:45 jioni kabla ya vikao kuanza.

Ndani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge, wageni wanapaswa kufuata na kuzingatia masharti yafuatatayo:-

Mambo yanayoruhusiwa Bungeni

· Kukaa kimya na kwa heshima inayostahili hadi watakapotoka nje ya ukumbi huo.

· Kuingia na kutoka Ukumbini kwa staha.

· Kuzima simu za mikononi.

· Kurejesha kitambulisho wakati wa kuondoka maeneo ya Bunge.

Mambo yasiyoruhusiwa Bungeni

· Hairuhusiwi kusoma kitabu chochote, gazeti, barua au hati nyingineyo ambayo si orodha ya shughuli za Bunge.

· Hairuhusiwi kuandika wala kurekodi jambo lolote linalozungumzwa, isipokuwa tu kama ni wawakilishi wa vyombo vya habari au maafisa wa serikali.

· Hairuhusiwi kuvuta sigara au kiko wakati wowote wakiwa ndani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge au mahali popote nje ya Ukumbi huo ambapo kuna mahali pa kukaa wageni.

· Hairuhusiwi kuingia na kamera wala kupiga picha kwa kutumia kifaa chochote kile.

· Hairuhusiwi kufanya jambo au kitendo chochote ambacho kinaweza kuvuruga amani na utulivu Bungeni.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's