Parliament of Tanzania

Waziri Mkuu amtakia Spika Kheri kwa Moyo wake wa Ukarimu

Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa amemtakia kheri Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai kwa moyo wake wa Ukarimu na kumuombea Kwa mwenyezi Mungu afanikishe shughuli zake zote anazozifanya.

Mheshimiwa Majaliwa alitoa kauli hiyo Mjini Dodoma jana wakati wa futari iliyoandaliwa na Mheshimiwa Ndugai kwa ajili ya waheshimiwa wabunge, wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge na baadhi ya Wazee wa Mkoa wa Dodoma shughuli iyofanyika katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

“Namshukuru Mheshimiwa Spika na Ofisi yake kwa ukarimu wa kuamua tupate futari leo, umetoa sadaka, Mwenyezi Mungu akuongezee Baraka ili uweze kufanikisha shughuli zako unazozifanya,” alisema.

Alisema hana mashaka na ukarimu wa Mheshimiwa Spika kwa kuwa tangu alipoingia Bungeni amekuwa na tabia hiyo ya kufuturisha kila mwaka katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Alisema hali hiyo inadhihirisha kwamba hafanyi kwa sababu ya dhama aliyonayo bali anafanya kwa dhamira yake ya dhati aliyonayo moyoni.

“Kwa dhamira yako hii, tunakushukuru na kukuombea kwa Mungu akuongozee pale ulipopunguza kwa kutoa,” alisema.

Aliwataka wale waliofunga na hata wale wasiofunga waendelee kuomba Mungu hasa katika kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's