United Republic of Tanzania
Parliament of Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
BUNGE LA TANZANIA
WARAKA WA SPIKA NA. 6/2017
KUHUSU
KUUNDWA KWA KAMATI MAALUM YA USHAURI KUHUSU NAMNA
YA KULIWEZESHA TAIFA KUNUFAIKA NA MAPATO YATOKANAYO
NA SEKTA NDOGO YA GESI
(Kanuni ya 5(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016)
_________________________
17 NOVEMBA, 2017
KUHUSU
KUUNDWA KWA KAMATI MAALUM YA USHAURI KUHUSU NAMNA
YA KULIWEZESHA TAIFA KUNUFAIKA NA MAPATO YATOKANAYO
NA SEKTA NDOGO YA GESI
(Kanuni ya 5(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016)
_________________________
(a) Utaratibu wa kuchangia gharama baina ya Serikali na mbia wake;
(b) Wabia kuwa na hisa za kipaumbele (Redeemed Preference Share) wakati Serikali ina hisa za kawaida;
(c) Uendeshaji wa Chombo cha Pamoja (Special Purpose Vehicle) ambapo Chombo hicho kinawaajiri wabia;
(d) Utaratibu wa kugawana gawio baina ya Serikali na mbia wake unaowapa wabia haki ya kupata gawio bila kujali faida inayopatikana na Serikali kupata gawio kutegemea faida itakayopatikana;
(e) Haki ya ushiriki wa wabia katika miradi inayotekelezwa (back-in-rights) kwa namna inayoinyima Serikali haki ya kushiriki katika uwekezaji;
(f) Ucheleweshaji wa tathmini na ukaguzi wa utekelezaji wa miradi ya mbia wa Serikali, jambo linaloathiri marekebisho ya dosari zinazobainika.
(a) Kubainisha dosari za kisera na sheria na kisheria katika kusimamia utekelezaji wa makubaliano ya uzalishaji wa pamoja na uendeshaji wa shughuli za utafutaji, uchimbaji na biashara ya gesi nchini;
(b) Kubainisha masharti hasi (Unconscionable terms) katika makubaliano na mikataba ya utafutaji na uchimbaji wa gesi nchini;
(c) Kupendekeza namna bora ya usimamizi na uendeshaji wa masuala ya gesi nchini;
(d) Kutoa mapendekezo kuhusu namna bora ya uingiaji wa mikataba ya uchimbaji, utafutaji na biashara ya gesi nchini; ; na
(e) Kushughulikia jambo jingine lolote linalohusiana na sekta ndogo ya gesi nchini.
(i) Mhe. Innocent Lugha Bashungwa, Mb.
(ii) Mhe. Dustan Luka Kitandula, Mb.
(iii) Mhe. Dkt. Suleiman Ally Yussuf, Mb
(iv) Mhe. Wanu Hafidh Ameir, Mb.
(v) Mhe. Oscar Rwegasira Mukasa, Mb.
(vi) Mhe. Ruth Hiyob Mollel, Mb.
(vii) Mhe. Richard Philip Mbogo, Mb.
(viii) Mhe. Omar Mohamed Kigua, Mb.
(ix) Mhe. Abdallah Ally Mtolea, Mb.
(x) Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mb.
(xi) Mhe. Doto M. Biteko, Mb - ambaye atakuwa Mwenyekiti
Uamuzi huu nautoa leo tarehe 17 Novemba, 2017
Mhe. Job Y. Ndugai, Mb.
SPIKA
17 Novemba, 2017