United Republic of Tanzania
Parliament of Tanzania
Spika wa Bunge
Mhe. Job Ndugai amekabidhiwa kitambulisho chake cha Taifa na Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba Mjini Dodoma ambacho kinaonesha picha yake, saini
yake pamoja na saini ya mtoa kitambulisho.
Mbali na Spika wa Bunge, Viongozi wengine waliochukua Vitambulisho vyao katika nyakati tofauti ni Naibu Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson, Mawaziri, Wabunge, Katibu wa Bunge na baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge.
Hatua
hiyo ya Spika Ndugai na Viongozi wengine kupokea Kitambulisho cha Taifa ni mkakati ambao
NIDA imekusudia kukamilisha usajili wa vitambulisho vya taifa nchi nzima kwa
wananchi, wageni na wakimbizi ifikapo Desemba mwaka huu pamoja na kutoa namba
ya utambulisho ambayo itawezesha makundi yote kupatahuduma mbalimbali.
Ili
kufikia malengo ya usajili wa ya kusajili Watanzania milioni 24, NIDA
imekusudia kutumia taarifa za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) milioni 22.7
ambazo watachakatwa na kutoa namba ya utambulisho (NIN) kabla ya kuzalisha
kitambulisho cha taifa.
Akizungumza
na waandishi wa habari mara baada ya kumkabidhi Spika kitambulisho hicho,
Waziri Mwigulu alisema kuwa kwa kutumia mfumo wa utambuzi na usajili wa watu
utasaidia kuwaunganisha wananchi na mifumo mingine ya huduma ikiwemo mifuko ya
hifadhi za jamii, benki, Bodi ya mikopo ya elimu ya juu, RITA na TCRA pamoja na
taasisi nyingine zinazotoa huduma.
Awali
Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano NIDA Bi. Rose Mdami amemueleza Spika Ndugai
kuwa vitambulisho hivyo vinaenda sambamba na mfumo wa utambuzi na usajili wa
watu utakaowaunganisha na mifumo mingine muhimu hapa nchini.
Bi. Mdami ameeleza kuwa mfumo huo umeunganishwa na Taasisi muhimu za Serikali ikiwemo TAMISEMI, TRA, TCRA, TASO, NEC, MDA, RITA, Polisi Uhamiaji, HELSB, Mifuko wa Hifadhi ya Jamii ili kuweza kuwa na taarifa za uhakika kwa Mhusika.
Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)
Special Seats (CCM)