Parliament of Tanzania

Mkutano wa Kumi wa Bunge waanza Mjni Dodoma

Mkutano wa Kumi wa Bunge la Kumi na Moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeanza leo Jumanne tarehe 30 Januari 2018 na unatarajiwa kumalizika tarehe 9 Februari 2018 Mjini Dodoma.


Mkutano huu umeanza kwa kushuhudia Wabunge wapya watatu waliochaguliwa hivi karibuni wakila Kiapo cha Uaminifu. Wabunge hao ni;

Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro – Songea Mjini.

Mhe. Monko Justine Joseph – Singida Kaskazini.

Mhe. Dkt. Stephano Lemomo Kiruswa – Longido.


Katika Mkutano huu wa Kumi, wastani wa maswali 125 ya Kawaida yanatarajiwa kuulizwa na Wabunge. Aidha, wastani wa Maswali 16 ya papo kwa papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu yanatarajiwa kuulizwa kwa siku ya Alhamisi tarehe 1 na 8 Februari,2018.


Kwa upande wa Miswada ya Serikali, Bunge pia linatarajia kupitisha kwa hatua zake zote Miswada Miwili ya Sheria ambayo ilisomwa Mara ya Kwanza katika Mkutano wa Tisa wa Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 91. Miswada hiyo ni :-


Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 5) wa Mwaka 2017 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 5) Bill, 2017].

Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma wa Mwaka 2017 [The Public Service Social Security Fund Bill, 2017].


Aidha, wakati wa Mkutano huu, Kamati 16 za Kudumu za Bunge zitawasilisha Taarifa zake Bungeni.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's