Parliament of Tanzania

Bunge laahirishwa hadi Januari 30, 2018

Mkutano wa Tisa wa Bunge la Kumi na Moja umeahirishwa hadi Januari 30, 2018 ambapo pamoja na mambo mengine, Bunge limetoa onyo kali pamoja na kuwaagiza Wahariri wa Magazeti ya Mtanzania, Mwananchi na Nipashe kuchapisha habari za kuomba radhi Bunge katika kurasa za mbele za magazeti yao ndani ya siku tano kuanzia tarehe ya Leo (17 Novemba, 2017,) kutokana na kosa la kuchapisha na kusambaza mwenendo wa shauri lililokuwa likifanyiwa kazi na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.


Adhabu hiyo imetolewa Bungeni leo wakati Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akitoa taarifa fupi kuhusu shauri la kuvunja Haki na Kinga za Bunge linalowahusu Wahariri na Waandishi wa Habari wa Magazeti ya Mtanzania, Mwananchi na Nipashe na kumuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali awafikishe Mahakamani Wahariri hao iwapo watashidwa kutekeleza agizo hilo ndani ya siku tano.


Mnamo tarehe 22 Septemba, 2017, magazeti hayo yalichapisha habari za mwenendo wa shauri na ushahidi uliotolewa na Mhe. Zitto Kabwe (Mb) mbele ya Kamati, kitendo ambacho ni kinyume na kifungu cha 34 (1) (f) na (g) ya Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge, Sura ya 296.

Kamati ya Maadili ilipendekeza na hatimaye Bunge kuridhia adhabu hiyo kwa wahusika baada ya kuzingatia kuwa Wahariri na Waandishi hao; waliitikia wito na kutoa ushirikiano kwa Kamati, walikiri na kujutia makosa yao na kwa kuwa ni wakosaji wa mara ya kwanza.


Wahariri na Waandishi wa Habari waliohojiwa na Kamati ya Maadili ni; Ndg. Denis Msacky, Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mtanzania, Ndg. Bakari Kimwanga, mwandishi wa habari wa gazeti la Mtanzania, Ndg. Angetile Osiah, Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwananchi, Ndg. Elias Msuya, mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Ndg. Edmond Msangi, Mhariri Mtendaji wa gazeti la Nipashe na Ndg. Gwamaka Alipipi, mwandishi wa habari wa gazeti la Nipashe.


Kuhusu Mheshimiwa Zitto, Spika wa Bunge aliliambia Bunge kuwa alitakiwa kufika mbele ya Kamati hiyo kwa mara nyingine kwa ajili ya mahojiano kutokana na vitendo vyake ya kuendelea kudharau Bunge, lakini bado hajaitikia wito na hivyo kwa wakati muafaka Kamati hiyo itamhoji na hatimaye kupeleka taarifa yake Bungeni kwa hatua zaidi.


Kwa upande mwingine Spika wa Bunge Mheshimiwa Ndugai kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa Kanuni ya 5(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, (Toleo la Januari, 2016,) ameunda Kamati maalum mbili za Ushauri kuhusu namna ya kuliwezesha Taifa kunufaika na sekta ndogo ya gesi na Kamati maalum ya Ushauri kuhusu namna kuliwezesha Taifa kunufaika na Sekta ya Uvuvi.


Kamati hizo mbili zimeelekezwa kufanya kazi kwa muda wa siku thelathini kuanzia tarehe watakayojulishwa na Katibu wa Bunge na baada ya kukamilisha kazi yake itawasilisha taarifa kwa Spika ili taratibu zingine muhimu zifuate.


Wajumbe walioteuliwa na Spika wa Bunge kuunda Kamati ya Ushauri kuhusu namna ya kuliwezesha Taifa kunufaika na sekta ndogo ya gesi ni pamoja na; Mhe. Innocent Lugha Bashungwa, Mb Mhe. Dustan Luka Kitandula, Mb, Mhe. Dkt. Suleiman Ally Yussuf, Mb, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, Mb, Mhe. Oscar Rwegasira Mukasa, Mb, Mhe. Ruth Hiyob Mollel, Mb; Mhe. Richard Philip Mbogo, Mb; Mhe. Omar Mohamed Kigua, Mb; Mhe. Abdallah Ally Mtolea, Mb; Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mb na Mhe. Doto M. Biteko, Mb - ambaye atakuwa Mwenyekiti.


Kwa upande wa kamati

ya Ushauri kuhusu namna ya kuliwezesha

Taifa kunufaika na sekta ya Uvuvi, Mheshimiwa Spika amewatea wajumbe wafuatao;

Mhe. Mussa Azzan Zungu, (Mb). Mhe. Salum Mwinyi Rehani, (Mb), Mhe. Masoud

Abdallah Salim, (Mb); Mhe. Tauhida Gallos Nyimbo, (Mb), Mhe. Mbaraka Kitwana

Dau, (Mb), Mhe. Dkt. Immaculate Sware Semesi, (Mb), Mhe. Dkt. Christine Gabriel

Ishengoma, (Mb), Mhe. Stanslaus Shing’oma Mabula, Mb, Mhe. Mussa Bakari

Mbarouk, (Mb), Mhe. Cosato David Chumi, (Mb) na Mhe. Anastazia Wambura, (Mb)- ambaye atakuwa Mwenyekiti.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

Member of the Parliament

Hon. Khalifa Salum Suleiman

Tunguu (CCM)

Profile

View All MP's